SIMBA SC YASONGA MBELE LIGI YA MABINGWA, SASA KUMENYANA NA PLATINUM FC YA ZIMBABWE


MABINGWA wa Tanzania, Simba SC wamefanikiwa kuingia Hatua ya 32 Bora michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya sare ya 0-0 na Plateau United ya Nigeria katika mchezo wa marudiano Raundi ya Awali leo Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.
Kwa matokeo hayo, Simba SC inasonga mbele kwa ushindi wa 1-0 ulioupata kutokana na bao pekee la Mzambia, Clatous Chama kwenye mchezo wa kwanza Jumapili iliyopita Uwanja wa Kimataifa wa Jos, Nigeria.
Sasa Wekundu wa Msimbazi watamenyana na Platinum FC ya Zimbabwe iliyoitoa Costa do Sol ya Msumbiji kwa jumla ya mabao 4-1 ikishinda 2-1 ugenini wiki iliyopita na 2-0 leo Bulawayo.  



Kikosi cha Simba SC kilikuwa; Aishi Manula, Shomari Kapombe, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, Erasto Nyoni, Pascal Wawa, Jonas Mkude, Hassan Dilunga/Bernard Morrison dk68, Muzamil Yassin, John Bocco, Clatous Chama na Luis Miquissone.
Plateau United; Adamu Abubakar, Abubakar Ibrahim, Gabriel Wassa, Dennis Nya, Andrew Ikefe, Isah Ndala, Oche Ochewechi, Sunday Adetunji, Abba Umar/Uche Onuasonya dk45, Ibrahim Buhari, Henlong Henry.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Contact Form