MANCHESTER CITY WAITANDIKA NEWCASTLE UNITED 2-0 ETIHAD




MABAO ya Ilkay Gundogan dakika ya 14 na Ferran Torres dakika ya 55 jana yaliipa Manchester City ushindi wa 2-0 dhidi ya Newcastle United katika mchezo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa Etihad. Kwa ushindi huo, kikosi cha Pep Guardiola kinafikisha pointi 26 baada ya kucheza mechi 14 na kusogea nafasi ya tano, sasa wakizidiwa pointi moja na mahasimu wao wa Jiji, Manchester United wanaoshika nafasi ya nne.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Contact Form